Mayalla ni wakili mashuhuri lakini amezungukwa na jamii
iliyomkaba kama ukono. Yeye angependa kuishi safi safina lakini
wakubwa wake kazini, wadogo wake, mkewe na hata abiria
anaosafiri pamoja nao katika daladala moja wana tofauti naye,
wote ni kama kaniki. Hawabadiliki na kutenda hata chembe ya
uadilifu. Ni waovu kinehe! Si maadili katika ndoa, si biashara, si
maamuzi ya mahakamani; yote ni hali moja, tenge tahanani. Je,
Mayalla ataiacha kazi ya serikali ili akimbilie Dubai na
kuyakwepa maovu yaliyomzunguka? Je, atabaki palepale katika
mzunguko wa dira ambao huishia dirani? Itambidi Mayalla
kupiga bongo ili kufanya maamuzi ya busara, kuiokoa jamii na
nafsi yake. La sivyo...
Hii ni riwaya ya kisasa kuhusu usasa na usasaleo wa jamii
iliyozingwa na maovu.